KIKAO KALI CHA 1
INGIA
(1 min)
Waruhusu washiriki wote na mwezeshaji waingie.
Or six.zume.training/checkin and use code: 1397
OMBA
(5 min)
Anza na maombi. Ufahamu wa kiroho na mabadiliko hayawezekani bila Roho Mtakatifu. Chukua muda kama kikundi kumwalika Yeye ili akuongoze katika kipindi hiki.
MAPITIO
(1 min)
Katika somo hili, tutasikia na kujadili dhana hizi:
Na tutaongeza zana hizi kwenye seti yetu ya zana:
- Mungu Anatumia Watu wa Kawaida
- Ufafanuzi rahisi wa Mwanafunzi na Kanisa
- Kupumua kwa Kiroho ni kusikia na kumtii Mungu
- Mtumiaji wa Maisha dhidi ya Watumiaji
- S.O.A.P.S. Kusoma Bibilia
- Makundi ya Uwajibikaji
- Jinsi ya kutumia Saa katika maombi
- Usimamizi wa Jamaa - Orodha ya 100
READ
(5 min)
Mungu Anatumia Watu wa Kawaida
Karibu kwenye mafundisho ya Zume. Zume ni neno la Kigiriki linalomaanisha "chachu."
Yesu anatuambia kwamba Ufalme wa Mungu ni kama mwanamke ambaye alichukua kiasi kidogo cha " Zume" na kukiweka kwenye kiasi kikubwa cha unga uliokandwa.
Alipokuwa akichanganya, chachu ilienea hata unga wote ukachachuka.
Yesu alikuwa anatufundisha kwamba mtu wa kawaida anaweza kutumia kitu kidogo sana na kusababisha kishindo kikubwa sana!
Ndoto yetu ni kufanya yale Yesu alisema -- kuwasaidia watu wa kawaida duniani kote kutumia vifaa vidogo kutoa vishindo vikubwa katika Ufalme wa Mungu!
Maagizo ya Yesu ya mwisho kwa wanafunzi wake yalikuwa rahisi. Alisema -- Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi -enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwa batiza kwa jina la baba, na la Mwana, nala Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Maagizo ya Yesu yalikuwa rahisi -Mkawafanye Wanafunzi
Amri yake jinsi ya kutekeleza hayo ilikuwa rahisi - mkafanye wanafunzi popote muendapo
- Mkafanye wanafunzi kwa kuwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu
- Mkawafanye wanafunzi kwa kuwafundisha yote niliyowaamuru
Kwa hivyo ni hatua zipi za kuwafanya wanafunzi?
- Tunawafanya wanafunzi kila wakati - popote tuendapo na tunapoenda
- Mtu akifanya uamuzi wa kumfuata Yesu - sharti abatizwe
- Wanapokua - tufundishe kila mwanafunzi jinsi ya kutii vitu vyote alivyoamuru Yesu.
Kwa vile kitu kimoja alichoamuru ni kufanya wanafunzi, hiyo inamaanisha kila mwanafunzi anayemfuata Yesu anastahili kujifunza jinsi ya kutengeneza wanafunzi pia.
Hao wanafunzi wanastahili kutengeneza wanafunzi. Na hao wanafunzi nao wakatengeneze wanafunzi, pia.
Kuzidisha wanafunzi. Hivyo ndivyo Zume inafanya kazi.
Ni kama chachu - ilijichanganya ndani mwa unga uliokandwa hadi wote ukawa chachu.
Wakati Yesu alipotoa amri hii ya kwenda kuwafanya wanafunzi, alitoa ahadi pia.
Yesu alisema - Nitakuwa nanyi daima. Hata ukamilifu wa dahari.
Kila mfuasi wa Yesu anapaswa kuzingatia ahadi ya kuwa Yesu yu pamoja nasi. Kwa sababu Yeye yuko!
Lakini pia inamaanisha kila mfuasi wa Yesu anapaswa kujitoa kwa ukweli kwamba Yesu anataka kila mmoja wetu atengeneneze wanafunzi. Kwa sababu Yeye alifanya.
Yesu alisema - nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi enendeni mkawafanye wanafunzi.
Mamlaka ambayo Yesu hutegemea wakati Anatutuma - ni mamlaka Yake
Yesu anasema hakuna mamlaka iliyo juu kuliko hiyo. Hakuna utamaduni uliyo na mamlaka zaidi.
Hakuna utamaduni uliyo na mamlaka zaidi. Hakuna sheria duniani iliyo na mamlaka zaidi.
Yesu alisema - nendeni mkawafanye wanafunzi.
Na kama Zume - chachu - tutaendelea kuenda na kukua hata kazi yote ikamilike.
JADILI
(10 min)
- Ikiwa Yesu alikusudia kila mmoja wa wafuasi Wake kutii Agizo Lake Kuu, kwa nini ni wachache sana wanaofanya wanafunzi?
READ
(5 min)
Wanafunzi na Kanisa
Karibuni tena kwenye mafundisho ya Zume.
Katika kipindi hiki, tutazungumzia kuhusu wanafunzi na kanisa.
Mwanafunzi ni nani?
Na wawezaje kumfanya mmoja? awe mwanafunzi kwa njia gani?
Je, wawezaje kumfundisha mfuasi wa Yesu kutii amri zake zote?
Je, unachukuliaje mtu ambaye aliishi maisha yake kama mtumwa wa ulimwengu na kumwezesha kuwa raia wa ufalme wa Mungu?
Maana ya neno mwanafunzi ni mfuasi.
Kwa hivyo mwanafunzi ni mfuasi wa Mungu.
Yesu alisema - Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
Kwa hivyo katika ufalme wa Mungu, Yesu ndiye Mfalme wetu.
Sisi ni raia wake, kwa mapenzi yake.
Wapenzi wake, makusudi, malengo yake, vipaumbele na maadili ni vya juu na bora zaidi.
Neno lake ni sheria. Kwa hivyo sheria ya ufalme ni nini? Je! Yesu anawaambia watu wake wakafanye nini?
Yesu alisema - Mpende Bwana Mungu kwa moyo wako wote, kwa nafsi yako yote, kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.
Yesu alisema - Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.
Yesu alisema kwamba amri za Mungu ktika Agano la Kale - sheria zote na manabii - zinaweza kufupishwa katika mambo haya mawili - mpende Mungu na Uwapende Watu
Yesu alisema - Fanya wanafunzi
Yesu alisema - Wafundishe kutii yote niliyoamuru.
Kwa kuwa kufanya wanafunzi inajumuisha kuwafundisha yote Yesu aliyoamuru - Agano Jipya inaweza kufupishwa kwa jambo moja - Wafanye Wanafunzi
Mwanafunzi ni mfuasi wa Yesu anayempenda Mungu, anapenda watu na huwafanya wanafunzi
Basi kanisa ni nini?
Huenda huwa unafikiria kanisa ni jengo - mahali unapoenda.
Lakini Neno la Mungu linazungumzia kanisa kama mkusanyiko - watu ambao wewe umo miongoni mwao.
Neno "kanisa" linatumiwa katika Biblia kwa njia tatu tofauti:
- kanisa la ulimwengu wote - watu wote ambao walikuwa, ambao wapo na ambao daima watakuwa wafuasi wa Yesu
- kanisa la jiji au la kanda - watu wote wanaomfuata Yesu na wanaishi humo au karibu na eneo fulani la ulimwengu
- kanisa la nyumbani - watu wote wanaomfuata Yesu na hukutana pahali mmoja ama watu wengi wanapoishi.
Familia ya kiroho - wafuasi wa Yesu wanaompenda Mungu, wanawapenda watu na kuwafanya wanafunzi ambao hukutana kwenye mitaa yao ndio aina ya mwisho ya kikundi hiki cha kanisa - kanisa la nyumbani au kanisa vivi hivi.
Wakati makundi ya makanisa haya yanapokutana kufanya kitu kikubwa, kwapamoja, wanaweza kutengeza kanisa la jiji au kikanda.
Makanisa hayo yote vivi hivi yameunganishwa katika mikoa na kuenea katika historia kufanya kanisa zima.
HILO NI KANISA NA HERUFI "K" KUBWA
Makanisa yakawaida ni familia za kiroho na Yesu kama kiungo cha kati na mfalme wao.
Makanisa ya kawaida ni familia za kiroho za wanaompenda Mungu, wanawapenda wengine na wanawafanya wanafunzi ambao wanajizidisha.
Makanisa mengine yana majengo na orodha na matumizi na wafanyi kazi. Lakini makanisa yakawaida hayana haja na vitu hivi ili wampende Mungu, wapende wengine na kuwafanya wanafunzi ambao wanajizidisha idadi.
Na kwa kuwa chochote cha ziada hulifanya kanisa kuwa na ugumu kujizidisha, mafundisho yetu huacha vitu kama majengo na orodha na matumizi na wafanya kazikwa kanisa la jiji la kanda lililojengwa kutokana na uzidishaji wa makanisa yakawaida.
Kumbuka kwamba "zume" inamaanisha "chachu" -- kiumbe ambacho kinazalisha haraka haraka.
Kupitia mafundisho ya Zume - tutakuwa kama ile chachu - vivi hivi na kujizidisha.
Lakini kabla tuanze kujizidisha -tuhakikishe kwamba tunajua kile Mungu anataka kizalishwe.
Kwa sababu kuzidisha kunaweza kuwa kuzuri - lakini sio kila mara.
Saratani hujizidisha. Na inaua.
Tunawezaje kuzalisha uhai na sio kifo? Tunawezaje kuhakikisha kwamba sisi ni wanafunzi wanaoweza kuzalisha?
JADILI
(10 min)
- Unapofikiria kuhusu kanisa, kitu gani huja mawazoni?
- Kuna tofauti gani kati ya picha hiyo na kile kinachofafanuliwa kwenye video kama "Kanisa Rahisi"?
- Unafikiri ni gani ingekuwa rahisi kuzidisha na kwa nini?
READ
(5 min)
Kumsikia na Kumtii Mungu
Karibu tena kwenye mafundisho ya Zume.
Katika kipindi hiki, tutaongea kuhusu kusikia kutoka kwa Mungu na kutii yale tunayosikia.
Kupumua ni maisha.
Tunavuta hewa ndani. Tunatoa hewa nje, ni uhai.
Kupumua ni muhimu katika Ufalme wa Mungu.
Kwa kweli, Mungu anaita Roho Wake - "pumzi"
Katika Ufalme, tunapumua ndani tunaposikia kutoka kwa Mungu.
Tunapumua wakati tunasikia kutoka kwa Mungu kupitia NENO LAKE - Biblia.
Tunapumua wakati tunaposikia kutoka kwa Mungu kupitia kwa MAOMBI - mazungumzo yetu naye.
Tunapumua wakati tunasikia kutoka kwa Mungu kupitia MWILI WAKE - kanisa, wafuasi wengine wa Yesu.
Tunapumua tunaposikia kutoka kwa Mungu kwa njia ya kazi zake - matukio, uzoefu na wakati mwingine hata mateso na kuteseka ambapo anaruhusu watoto wake kupitia.
Katika Ufalme tunapumua NJE tunapotenda kwa ajili ya yale tunasikia kutoka kwa Mungu. Tunapumua NJE wakati TUNATII.
Wakati mwingine kupumua nje kwa KUTII inamaanisha kubadilisha mawazo yetu, maneno yetu au matendo yetu ili kuwaleta pamoja na Yesu na mapenzi Yake.
Wakati mwingine kupumua kwa KUTII kunamaanisha kugawana kile Yesu ameshiriki nasi - kupeana kile alichotupa - ili wengine waweze kubarikiwa kama vile Mungu anavyotubariki.
Kwa mfuasi wa Yesu - hii kupumua NDANI na kupumua NJE ni muhimu. Ni maisha yetu.
Yesu alisema - Mwana hawezi kufanya kitu peke yake. Anafanya tu yale anayoyaona Baba akifanya. Chochote Baba anachofanya, Mwana pia hufanya.
Yesu alisema - Sineni kwa mamlaka yangu mwenyewe. Baba aliyenituma ameniamrisha cha kusema na jinsi ya kusema.
Yesu alisema kwamba kila neno alilosema na kila kazi aliyotimiza ilitokana na KUSIKIA kutoka kwa Mungu na KUTII yale aliyasikia.
Pumua NDANI - Sikia kutoka kwa Mungu.
Pumua NJE - Tii yale unayosikia na ushiriki na wengine.
Yesu alisema kwamba wafuasi wake pia watasikia kutoka kwa Mungu kwa sababu ya Roho Mtakatifu wake - Kupumua Kwake - ambayo itapumuliwa ndani ya kila mmoja wetu anayemfuata.
Yesu alisema - Msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisha vitu vyote na kuwakumbusheni kila kitu nilichowaambia.
Kupumua NDANI- Sikia kutoka kwa Mungu.
Pumua NJE- Tii yale unayoyasikia na uishiriki na wengine.
Yesu alikuwa anatuonyesha jinsi ya kuishi.
Kwa hivyo tunaisikiaje sauti ya Mungu? Tunajuaje nini cha kutii?
Yesu alijiita mwenyewe "Mchungaji Mzuri". Yesu aliwaita wafuasi "kondoo"wake.
Yesu akasema - Kondoo wangu husikia sauti Yangu, na ninawajua, na wananifuata.
Yesu alisema - Yeyote aliye wa Mungu husikia kile ambacho Mungu anasema. Sababu hamsikii ni kwamba ninyi si wa Mungu.
Kama wafuasi wa Yesu, tunapaswa kujitolea kusikia sauti Yake.
- TUNASIKIA sauti yake kwa kuwa kimya.
- TUNASIKIA sauti yake kwa kumzingatia Yesu.
- TUNASIKIA sauti yake katika mawazo yetu, maono yetu, hisia zetu na dhana zetu.
- TUNASIKIA sauti yake tunapoandika na kuhakiki kile tunachosikia.
Si kila sauti, sio kila wazo, sio maono, hisia au dhana ni sauti ya Mungu.
Wakati mwingine ni sauti ya adui
Yesu alisema adui yetu ni mwongo na baba wa uongo. Yesu alisema adui yetu huja kuiba, kuua na kuharibu.
Lakini Mungu anasema kwamba TUTASIKIA kutoka kwake na tutajua ni Yeye wakati anapozungumza
Kwa kujizoeza na maombi, tunaweza kujua sauti ya Mungu vyema. Tunaweza kujifunza kujua kama tunachosikia ni kutoka kwa Mungu au sauti nyingine.
Hapa kuna njia ya kujaribu yale tunayosikia:
- Wakati Yesu anapoongea - sauti yake itakuwa thabiti Neno lake Lililoandikwa -
- Biblia - tayari imetueleza. Sauti yake haitakinzana na sauti ilioandikwa.
- Wakati Yesu anapoongea - sauti yake itaipa mioyo yetu hisia ya tumaini na amani. Sauti yake haitatuacha ama kutuvunja mioyo. Yesu hahukumu. Yesu hurekebisha kwa upendo.
- Sauti ya Yesu haitaelezea matendo ya mwili - uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu na uchawi, uadai, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, mambo haya sio sauti ya Mungu.
- Wakati Yesu anapoongea - sauti yake itatuonyesha matunda ya Roho wa Mungu - upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi.
Wakati Yesu akisema - Sauti yake hutupa hisia za kujiamini badala ya wasiwasi. Tunapata ndani mwetu ujuzi na amani kwamba kile tunachosikia kinatoka kwa Mungu. Hatuwezi kusikia kila kitu mara moja. Tunaweza kusikia sehemu tu ya kile tunachohitajika kujua. Lakini kile tunasikia itakuwa imara - si ya kuhama hama au kujibadilisha.
Habari njema kwa kila mfuasi wa Yesu ni kwamba tunapopumua NDANI na KUSIKIA kutoka kwa Mungu na tunapopumua NJE na KUTII tunachosikia na kushirikiana na wengine tulichosikia - Mungu ataongea wazi wazi.
Pumzi yake itapumua kupitia sisi hata zaidi.
TUTASIKIA sauti yake wazi zaidi.
TUTAJUA sauti yake na sio nyingine.
TUTAONA kazi ndani yake duniani na kujiunga naye kufanya kazi pamoja
Tunapumua. Tunapumua nje. Uzima.
JADILI
(10 min)
- Kwa nini ni muhimu kujifunza na kusikia na kutambua sauti ya Mungu?
- Je, kusikia na kumuitikia Bwana ni kama kupumua? Kwa nini au kwa nini sivyo?
READ
(5 min)
S.O.A.P.S. Kusoma Bibilia
Yesu alisema --"mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi…"
Ikiwa kila mfuasi wa Yesu atatii yote ambayo Yesu aliamuru, atahitaji kujua kile Yesu alichoamuru.
Amri Kuu na Agizo Kuu ni muhtasari mkuu wa kile Mungu anatuambia, lakini ili mfuasi akue kikamilifu na awe kile ambacho Mungu alimuumba kuwa, anahitaji kuwa na ufahamu na kutii hata zaidi.
S.O.A.P.S. inamaanisha:
- Maandiko
- Uchunguzi
- Matumizi
- Sala na
- Kushiriki
Ni njia rahisi ya kujifunza na kukumbuka mbinu ya kujifunza Biblia yenye ufanisi ambayo mfuasi yeyote wa Yesu anaweza kutumia. Hebu tuangazie kile sehemu kwa undani zaidi.
Unaposoma au kusikiliza Biblia:
- Maandiko : Andika mstari mmoja au zaidi ambayo ina umuhimu kwako zaidi, leo.
- Uchunguzi : Andika tena mistari hiyo kutoka kwenye Maandiko hayo kwa maneno yako mwenyewe ili kukusaidia kuelewa vyema zaidi maana iliyoko.
- Matumizi : Tafakari maana ya kutii amri au dhana hizo katika maisha yako mwenyewe. Utahitaji kufanya nini kwa njia tofauti? Andika mambo hayo.
- Sala : Andika sala inayomwambia Mungu kile ambacho umekuwa ukisoma katika Neno lake na kile unachoelewa kuhusu kutii amri zake na kutekeleza kile ulichojifunza.
- Kushiriki : Muulize Mungu anataka ushiriki na nani kile ulichojifunza na jinsi unavyokitumia.
Basi hebu tutumie S.O.A.P.S:
- Maandiko - Biblia inasema: "Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu," asema BWANA. "Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu." Isaya 55:8-9
- Uchunguzi - Kama mwanadamu, nina mipaka katika kile ninachojua na kile ninachojua jinsi ya kukifanya. Lakini Mungu hana mipaka yoyote. Anaona na anajua kila kitu. Anaweza kufanya lolote lile.
- Matumizi - Kwa vile Mungu anajua kila kitu na njia zake ndio bora zaidi, nitapata mafanikio zaidi maishani ikiwa nitamfuata badala ya kutegemea njia yangu ya kufanya mambo.
- Sala - Bwana, sijui jinsi ya kuishi maisha mazuri yanayokupendeza na yanayosaidia wengine. Njia zangu husababisha makosa. Mawazo yangu husababisha maumivu. Naomba unifundishe njia zako na mawazo yako badala yake. Roho wako Mtakatifu aniongoze ninapokufuata.
- Kushiriki - Nitashiriki mistari hii na matumizi yake na rafiki yangu, Steve, ambaye anapitia wakati mgumu na anahitaji mwongozo kwa ajili ya maamuzi muhimu yanayomkabili.
Kujifunza Biblia Kupitia S.O.A.P.S. Mojawapo ya zana rahisi katika Seti Yetu ya Zana ya Zume.
SHUGHULI
(30 min)
Kichwa: Somo la Biblia la SOAPS
MAUDHUI:
Maandiko
Andika mstari mmoja au zaidi ambayo ni ya maana sana kwako, leo.
Uchunguzi
Andika upya mistari hiyo au mambo muhimu kwa maneno yako mwenyewe ili kuelewa vyema.
Utendaji
Fikiria juu ya nini maana ya kutii amri hizi katika maisha yako mwenyewe.
Maombi
Andika maombi ukimwambia Mungu yale uliyojifunza na jinsi unavyopanga kutii.
Kushikiri
Muulize Mungu ambaye anataka ushiriki naye kuhusu yale uliyojifunza/kutumia.
Hapa kuna mfano wa S.O.A.P.S. kazini:
S - "Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu," asema Bwana. "Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu." Isaya 55:8-9
O - Kama binadamu, nina mipaka katika kile ninachojua na kile ninachojua kufanya. Mungu hana kikomo kwa njia yoyote. Anaona na anajua YOTE. Anaweza CHOCHOTE.
A - Kwa kuwa Mungu anajua kila kitu na njia zake ni bora zaidi, nitakuwa na mafanikio zaidi maishani ikiwa nitamfuata badala ya kutegemea njia yangu mwenyewe ya kufanya mambo.
P - Bwana, sijui jinsi ya kuishi maisha mazuri yanayokupendeza na kusaidia wengine. Njia zangu husababisha makosa. Mawazo yangu husababisha maumivu. Tafadhali nifundishe njia Zako na mawazo Yako, badala yake. Acha Roho wako Mtakatifu aniongoze ninapokufuata Wewe.
S - Nitashiriki mistari hii na matumizi haya na rafiki yangu, Steve, ambaye anapitia wakati mgumu na anahitaji mwelekeo wa maamuzi muhimu anayokabili.
READ
(5 min)
Makundi ya Uwajibikaji
Yesu alisema -"Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi."
Yesu alisimulia hadithi nyingi kuhusu uwajibikaji na alituambia kweli nyingi kuhusu jinsi tutakavyowajibishwa kwa kile tunachofanya na kusema.
Yesu anatuambia mambo haya sasa, ili tuwe tayari kwa ajili ya baadaye. Na kwa vile tutawajibishwa mbele zake siku moja, ni vyema kuwa na tabia ya kuwajibishana sasa.
Makundi ya Uwajibijaki yanaundwa na watu wawili au watatu wa jinsia moja- wanaume kwa wanaume, wanawake kwa wanawake - wanaokutana mara moja kwa wiki kujadili seti ya maswali yanayosaidia kufichua sehemu ambapo mambo yanaenda vizuri na sehemu zingine zinazohitaji marekebisho.
Kila mfuasi wa Yesu atawajibishwa, hivyo kila mfuasi wa Yesu anapaswa kuwajibika kwa wengine.
Makundi ya Uwajibikaji Zana nyingine rahisi katika Seti Yetu ya Zana ya Zume.
SHUGHULI
(20 min)
Jina: vikundi vya uwajibikaji
Maudhui:
- Umemuonaje Mungu akifanya kazi?
- Je, umekuwa ushuhuda wiki hii kwa ukuu wa Yesu Kristo kwa maneno na matendo yako yote?
- Je, umekabiliwa na nyenzo zinazovutia ngono au kuruhusu akili yako kuwaza mawazo yasiyofaa ya ngono?
- Je, umekubali umiliki wa Mungu katika matumizi yako ya pesa?
- Umetamani chochote?
- Je, umeumiza sifa au hisia za mtu kwa maneno yako?
- Je, umekuwa si mwaminifu kwa maneno au matendo au kutia chumvi?
- Je, umejihusisha na tabia ya uraibu (au mvivu au isiyo na nidhamu)?
- Je, umekuwa mtumwa wa mavazi, marafiki, kazi, au mali?
- Umeshindwa kumsamehe mtu?
- Je, ni wasiwasi gani au wasiwasi gani unaokumbana nao?
- Je, umelalamika au kunung'unika?
- Je, umedumisha moyo wa shukrani?
- Je, umekuwa ukiheshimu, kuelewa na kuwa mkarimu katika mahusiano yako muhimu?
- Je, ni majaribu gani katika mawazo, neno, au matendo ambayo umekumbana nayo na ulijibu vipi?
- Je, umechukuaje fursa za kuwatumikia au kuwabariki wengine, hasa waumini?
- Je, umeona majibu mahususi kwa maombi?
ANGALIA
(1 min)
Dhana zilizosikika katika kikao hiki:
Zana zilizosikika katika kikao hiki:
- Mungu Anatumia Watu wa Kawaida
- Ufafanuzi rahisi wa Mwanafunzi na Kanisa
- Kupumua kwa Kiroho ni kusikia na kumtii Mungu
- Mtumiaji wa Maisha dhidi ya Watumiaji
- S.O.A.P.S. Kusoma Bibilia
- Makundi ya Uwajibikaji
- Jinsi ya kutumia Saa katika maombi
- Usimamizi wa Jamaa - Orodha ya 100
Take a Break
MAPITIO
(1 min)
Katika somo hili, tutasikia na kujadili dhana hizi:
Na tutaongeza zana hizi kwenye seti yetu ya zana:
- Mungu Anatumia Watu wa Kawaida
- Ufafanuzi rahisi wa Mwanafunzi na Kanisa
- Kupumua kwa Kiroho ni kusikia na kumtii Mungu
- Mtumiaji wa Maisha dhidi ya Watumiaji
- S.O.A.P.S. Kusoma Bibilia
- Makundi ya Uwajibikaji
- Jinsi ya kutumia Saa katika maombi
- Usimamizi wa Jamaa - Orodha ya 100
READ
(5 min)
Mtayarishaji sio Mtumiaji
Katika kikao hiki, tutazungumzia kuhusu jinsi tunaweza kumsaidia mfuasi wa Yesu kuwa MZALISHAJI katika ufalme wa Mungu badala ya mlaji tu.
Katika mpango wake mkamilifu, Mungu alituumba tuishi katika usawa - KUZAANA na KULA, KUFANYIZA na KUTUMIA, KUMWAGA NJE na KUJAZWA ili tuweze KUMWAGA NJE tena.
Lakini, katika dunia yetu hii, watu wamekataa mpango wake Mungu, na wengi wanatumia nguvu zao kuishi nje ya sehemu ya ulinganisho wa Mungu.
WANAJIFUNZA bali hawashirikiani. WAMEJAZWA bali hawamwagi nje. WANATUMIA bali hawazilishi.
Ikiwa tutawafanya wanafunzi wanaojizidisha, basi tunahitaji kushiriki pamoja nao jinsi wanaweza kuwa wazalishaji na sio watumiaji tu.
Tunaweza kufanya hivyo hapa - Mungu anatumia Neno lililoandikwa - ambalo tunaita maandiko ama Biblia - ili kukua kiroho.
Kila mwanafunzi anahitaji kujiandaa ili akasome, kutafsiri na kutumia maandiko.
Zaidi ya maelfu ya miaka na kwa mikono ya waandishi wengi tofauti, Mungu alinena neno lake ndani ya mioyo ya watu waaminifu ambao walishika na kushirikiana yale waliyoyasikia.
Maandiko yanatufundisha hadithi ya Mungu, mipango yake, moyo wake, njia zake.
Katika kikao cha awali, mlijifunza kuhusu vyombo viwili - masomo ya Biblia ya SOAPS na Kikundi cha Uwajibikaji. Katika kikao kijacho, mtajifunza chombo kimoja kingine - vikundi vya theluthi 3/3.
Vifaa hivi vitatu vinafanya kazi kwa pamoja ili kusaidia wafuasi wapya kujifunza, kutafsiri na kutumia Neno la Mungu lililoandikwa.
Watajifunza sio kuwa tu wasikizaji wa Neno la Mungu bali watendaji na washirika, pia.
Mungu hutumia Neno lake Lililonenwa - ambalo unaweza kutambua kwa njia ya maombi - kutufanya tukue kiroho.
Maombi ni kuzungumza na kumsikiliza Mungu. Maombi hutusaidia kumjua Mungu kwa ukaribu sana na kuelewa moyo wake, mapenzi yake na njia zake.
Maombi hutusaidia katika huduma na kuwatumikia wengine, hutusaidia kufundisha na kushiriki katika njia maalum ambayo husaidia mtu au kikundi kumjua Mungu vizuri.
Vifaa viwili - Kuomba kwa kutembea na kuomba kwa mviringo huwasaidia Wafuasi kuendeleza maombi ya kibinafsi na kujifunza maisha ya maombi ya kibinafsi na kuomba kwa njia ambazo zinahudumia wengine.
Vifaa hivi husaidia kuendeleza tabia ya kuomba bila kukoma na kujifunza kuona dunia kutokana na mtazamo wa kiroho badala ya kutegemea yale tunayoweza kuona tu.
Ikitumika kwa uthabiti, vinasaidia mfuasi wa Yesu, kuongeza uwezo wao wa maombi na kuongeza uwezo wao wa kusikia kutoka kwa Mungu na kushirikiana yale wanayoyasikia.
Mungu hutumia waumini Mwili wake - ambao tunaita Kanisa ama Wafuasi wa Yesu - kutukuza kiroho.
Kama mkusanyiko wa waumini, tumeunganishwa. Neno la Mungu linasema kwamba, katika Yesu - sisi ni sehemu nyingi za mwili mmoja, na tunahusiana. Kwa maneno mengine, hatujaunganishwa tu na Mungu - tumeunganishwa na kila mmoja.
Mungu anasema mjiwasilishe kila mmoja kwa mwenzake. Mungu anasema mkahudumiane.
Kila mmoja wetu ana uwezo tofauti na kila mmoja ana udhaifu. Mungu anatutarajia sisi kuwaruhusu wengine kutusaidia katika udhaifu wetu kwa kutumia uwezo aliyowapa.
Neno la Mungu iinasema Mungu amempa kila mmoja uwezo wa kipekee; zitumie kuwasaidia wengine, kuwapa wengine baraka nyingi za Mungu.
Vifaa vingi kama vile vikundi vya theluthi 3/3, vikundi vya uwajibikaji na Kushauriana Ki rika hutusaidia kuhimizana mmoja kwa mwenzake kiupendo na kazi nzuri sio tu kutusaidia kutii yale Mungu anatueleza kufanya bali inatusaidia kupata njia ya kushiriki na wengine yale tuliyojifunza na wengine.
Mungu pia hutumia udhalimu na mateso - dhabihu na hasara tunayokabiliana nayo kwa ajili ya Yesu - kutufanya tukue kiroho.
Wakati watu wanatuhukumu na kutuumiza kwa sababu tunampenda na kumtii Yesu, ama wakati mambo mabaya yanatutokea pamoja na kwamba tunampenda na kumtii Yesu, Mungu hutumia huo udhalimu na mateso kuboresha tabia zetu kutufanya tuwe kama Yesu.
Yeye hustawisha tabia zetu, hutuimarisha na kutakasa imani yetu, hutuandaa kwa huduma na hutuwezesha kuhudumia wegine ambao wanateseka - wakati wote akijitambulisha waziwazi kwa kila mtu anayetutazama na kuelewa maumivu yetu.
Mungu anatueleza kwamba, kama wafuasi wa Yesu lazima tutarajie mateso.
Yesu alisema - Mungu atawabariki wakati watu wanakutukana, wanakutendea mabaya, na kusema kila aina uongo juu yenu kwa ajili yangu mimi. Kueni na furaha na msisimko! Mtakuwa na thawabu kubwa mbinguni. Watu waliwafanyia mambo hayo manabii ambao waliishi zamani.
Vifaa kama theluthi 3/3 vya vikundi vya uwajibikaji huwapa wafuasi wa Yesu fursa ya kushiriki udhalimu na mateso wanayopata.
Vikundi hivi vinawapa nafasi ya kufundisha wanafunzi kwamba neno la Mungu linasema tutarajie nyakati ngumu na kuwawezeshea njia ambazo wanaweza kukabiliana nazo kwa kuamini upendo wake Mungu hata wakati mambo yanaenda mrama.
Maandiko. Maombi. Mwili Uzima. Udhalimu na Mateso.
Hivi ndivyo Mungu anatukuza tue bora zaidi kama mwanawe mkamilifu Yesu.
Vifaa vinavyotusaidia sio tu kwa watumiaji wa mambo haya mazuri ambayo Mungu ametupa bali kuwa wazalishaji na washirika pia
JADILI
(10 min)
- Katika maeneo manne yaliyo hapo juu (maombi, Neno la Mungu, nk), ni ipi tayari unafanya?
- Ni zipi unahisi huna hakika nazo?
- Je! Unajisikia tayari kiasi wakati wa kufundisha wengine?
READ
(5 min)
Mfuatano wa Maombi
Yesu mara nyingi alifundisha wafuasi wake kuhusu kusudi, desturi na ahadi za sala.
Yesu alisema -"Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa."
Yesu aliwafundisha wafuasi wake kwamba sala si kwa ajili ya kusifiwa na watu, si kuomba vitu kwa ubinafsi wala si hotuba ndefu isiyo na mwelekeo tunayorudia tena na tena.
Yesu alituonyesha kwamba sala ina nguvu kwa sababu ni mazungumzo ya moja kwa moja yasiyokoma na Baba yetu wa mbinguni atupendaye. Kama mazungumzo yoyote mazuri, sala nzuri inamaanisha kwamba pande zote mbili zinasikiliza -- na kuzungumza. Lakini kuzungumza na Mungu aliyeumba ulimwengu kunaweza kuogopesha. Na kusikia akisema kitu - kwa watu wengi hilo linaweza kushtua sana.
Habari njema ni kwamba kuwa na ustadi katika sala -kuwa na mazungumzo bora na ya kina zaidi na Mungu atupendaye - si tu jambo linalowezakana -bali pia ni jambo analotaka Mungu.
Lakini sala inapohisi kama kujifunza lugha mpya -Utakuwaje na ustadi? Jibu ni rahisi - unajizoeza. Mzunguko wa Sala ni zana rahisi ya kujizoeza sala ambayo unaweza kutumia na kushiriki na mfuasi mwingine.
Kwa hatua 12 tu rahisi - kila moja ikihitaji dakika 5 - Mzunguko wa Sala unakuongoza katika hatua kumi na mbili ambazo kwazo Biblia inatufundisha kuomba. Mwishowe, utakuwa umeomba kwa saa moja. Biblia inatuambia - "Ombeni bila kukoma." Si wengi wetu tunaweza kusema tunafanya hivyo. Lakini katika saa hii moja ya sala - utakuwa umepiga hatua mbele.
Mzunguko wa Sala - Zana nyingine moja zaidi rahisi katika Seti Yetu ya Zana ya Zume.
SHUGHULI
(60 min)
Kichwa: Mzunguko wa Maombi
Maudhui:
Kwa hatua 12 tu rahisi - dakika 5 kila moja - Mzunguko huu wa Maombi unakuongoza kupitia njia 12 ambazo Biblia inatufundisha kuomba. Mwishowe, utakuwa umeomba kwa saa moja.

SIFA
Anza saa yako ya maombi kwa kumsifu Bwana. Msifu kwa mambo ambayo yako akilini mwako sasa hivi. Msifu kwa jambo moja maalum ambalo amefanya katika maisha yako katika wiki iliyopita. Msifu kwa wema wake kwa familia yako.
SUBIRI
Tumia muda kumngoja Bwana. Nyamaza na umruhusu akuvute tafakari.
UKIRI
Mwombe Roho Mtakatifu akuonyeshe chochote katika maisha yako ambacho kinaweza kuwa hakimpendezi. Mwambie akuonyeshe mitazamo ambayo si sahihi, pamoja na matendo mahususi ambayo bado hujafanya maombi ya kuungama. Sasa ungameni hilo kwa Bwana ili mpate kutakaswa.
SOMA NENO
Tumia muda kusoma katika Zaburi, katika manabii, au vifungu vya maombi vilivyo katika Agano Jipya.
ULIZA
Fanya maombi kwa niaba yako mwenyewe.
MAOMBI
Fanya maombi kwa niaba ya wengine.
OMBA NENO
Omba vifungu maalum. Sala za Kimaandiko na vilevile Zaburi kadhaa hufaa kwa kusudi hilo.
ASANTE
Mshukuru Bwana kwa mambo katika maisha yako, kwa niaba ya familia yako, na kwa niaba ya kanisa lako.
IMBA
Imba nyimbo za sifa au kuabudu au wimbo mwingine au wimbo wa kiroho.
TAFAKARI
Mwombe Bwana aseme nawe. Kuwa na kalamu na karatasi tayari kurekodi hisia Anazokupa.
SIKILIZA
Tumia muda kuunganisha mambo ambayo umesoma, mambo ambayo umeomba na mambo ambayo umeimba na uone jinsi Bwana anavyovileta pamoja ili kuzungumza nawe.
SIFA
Msifu Bwana kwa muda ambao umekuwa naye na hisia ambazo amekupa. Msifuni kwa sifa zake tukufu.
Kutoka kwenye kitabu cha Dick Eastman cha The Hour that Changes the World (C) 2002 na Dick Eastman, Chosen Books, Grand Rapids, MI, kilichotumiwa kwa ruhusa.
JADILI
(10 min)
- Je, unaonaje kutumia lisali moja kwa maombi?
- Unahisi aje?
- Ulijifunza au kusikia chochote?
- Je! Maisha yangekuwaje kama ungefanya maombi ya aina hii kuwa kawaida?
READ
(5 min)
Orodha ya 100
Yesu alisema - "Nendeni mkafanye wanafunzi…" Na wafuasi wake walifanya vivyo hivyo.
Walienda kwa familia zao. Walienda kwa marafiki zao. Walienda kwa watu waliowajua mjini. Walienda kwa watu waliofanya kazi nao. Walienda.
Yesu alisema "Nendeni" nao wakatii. Na familia ya Mungu ikakua.
Mungu tayari ametupatia mahusiano tunayohitaji ili "twende na kufanya wanafunzi." Hao ni familia zetu, marafiki, majirani, wafanyakazi wenzetu na wanafunzi wenzetu - watu ambao tumewajua maisha yetu yote, watu ambao tumewajua hivi karibuni.
Kuwa waaminifu na watu ambao Mungu tayari ameweka maishani mwetu ni hatua nzuri ya kwanza katika kuzidisha wanafunzi. Na unaweza kuanza na hatua rahisi ya kuandika orodha.
Orodha ya watu 100 ni zana rahisi katika Seti Yetu ya Zana ya Zume inayozidisha wanafunzi.
SHUGHULI
(30 min)
Tengeneza orodha yako mwenyewe ya mia moja
Tengeneza orodha yako ya usimamizi wa mahusiano: andika watu walio katika miduara yako ya ushawishi. Weka alama kuonyesha ikiwa kila mtu ni mfuasi, bado si mwamini, au hajulikani.
Tumia muda kama kikundi ili kila mtu ajenge orodha yake mwenyewe. Unaweza kutumia karatasi au zana za kidijitali katika vifaa vyako vya mafunzo.
ANGALIA
(1 min)
Dhana zilizosikika katika kikao hiki:
Zana zilizosikika katika kikao hiki:
- Mungu Anatumia Watu wa Kawaida
- Ufafanuzi rahisi wa Mwanafunzi na Kanisa
- Kupumua kwa Kiroho ni kusikia na kumtii Mungu
- Mtumiaji wa Maisha dhidi ya Watumiaji
- S.O.A.P.S. Kusoma Bibilia
- Makundi ya Uwajibikaji
- Jinsi ya kutumia Saa katika maombi
- Usimamizi wa Jamaa - Orodha ya 100